AudioPlayer


-->



jinsi maombi yanavyobalisha


JINSI KUFUNGA KUNAVYOBADILISHA

MAMBO

Sehemu nyingi sana katika Biblia, tunaona

jinsi ambavyo mambo yalivyobadilika

baada ya kufunga na kuomba. Angalia

mifano mitano ifuatayo:-

1. Wana wa Israeli walipigwa mfululizo

katika vita na wana wa Benyamini. Baada

ya kushindwa mfululizo, wakaamua

kufunga na kuomba (WAAMUZI 20:20-22,

24-26). Baada ya kufunga na kuomba

matokeo yakabadilika, Benyamini

wakapigwa sana, na wana wa Israeli

wakashinda vita (WAAMUZI 20:34-35, 41-45,

48). Tunaweza kuitia moto miji yote ya

Shetani tukiwa wafungaji, na siyo kinyume

cha hapo;

2. Ezra hakumtegemea mfalme, bali

alifunga, na matokeo ya kufunga yakawa

kwamba mkono wa Mungu ulikuwa pamoja

naye na yeye na wenzake wakaokolewa na

mkono wa adui (EZRA 8:21-28, 31-33). Ikiwa

Kanisa linahitaji kuokolewa kutoka katika

mkono wa adui, ni lazima liwe na

wafungaji.

3. Yehoshafati alipata taarifa za majeshi

kombaini ya Maadui waliotaka kumpiga.

Akatangaza kufunga na kuomba (2 MAMBO

YA NYAKATI 20:1-4), matokeo yake

wakashinda vita kirahisi mno kwa sifa tu (2

MAMBO YA NYAKATI 20:22-25).

4. Nehemia alivyopata taarifa za

kubomolewa kwa ukuta wa Yerusalemu na

malango yaliyoteketezwa kwa moto,

alifunga na kuomba (NEHEMIA 1:3-4), na

matokeo yake ukuta ulijengwa tena

(NEHEMIA 6:15-16).

5. Hasira ya Bwana kwa Kanisa, Taifa,

kutokana na uovu wa watu, inaweza

kufanywa kuwa AMANI kwa KUFUNGA NA

KUOMBA (1 WAFALME 21:27-29; YONA

3:7-10; EZRA 10:6).

Hakuna maoni: